Rasmi: Chelsea yaorodhesha wachezaji 23 watakaoshiriki Europa League - Darajani 1905

Rasmi: Chelsea yaorodhesha wachezaji 23 watakaoshiriki Europa League

Share This
Kati ya michuano ambayo Chelsea inashiriki msimu huu ni.michuano ya ligi ya Ulaya maarufu kama Europa League ambayo itaanza kutimua vumbi tarehe 24 ya mwezi huu Septemba.

Kuelekea kwenye michuano hiyo, klabu zinatakiwa kuorodhesha majina ya wachezaji wake ambao itawatumia katika michuano hiyo kwa msimu mzima. Na tayari klabu ya Chelsea imeshaorodhesha majina ya nyota 23 itakaowatumia kwenye michuano hiyo.

Kikosi kamili:
Makipa: Kepa Arrizabalaga na Willy Caballero
Walinzi: Ethan Ampadu, Cesar Azpilicueta, Antonio Rudiger, David Luiz, Marcos Alonso, Emerson Palmieri, Andreas Christensen na Gary Cahill
Viungo: Ruben Loftus-Cheek, Ross Barkley, Victor Moses, N'Golo Kante, Jorginho Frello, Danny Drinkwater, Mateo Kovacic na Cesc Fabregas
Washambuliaji: Eden Hazard, Olivier Giroud, Alvaro Morata, Pedro Rodriguez na Willian Borges.

Muhimu ni kutambua kwamba nyota hawa watatumika kama wachezaji wa Chelsea kwa msimu mzima wa michuano ya Ulaya na endapo ikatokea amejiunga na klabu nyengine basi hatoruhusiwa kushiriki ama michuano ya Klabu bingwa barani Ulaya au ligi ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment