About Us - Darajani 1905

About Us

Ukurasa wa Darajani 1905 ni ukurasa ulioanzishwa rasmi tarehe 19-Desemba-2017 na kiongozi wake mkuu ni Barnabas Gwakisa Mwamusaku ambaye kama shabiki wa Chelsea aliona ni vyema kuwa na ukurasa utakaokuwa unatoa habari zote za Chelsea kwa lugha ya Kiswahili ili kuwapatia habari na ufafanuzi wa kina mashabiki wa klabu hiyo lakini pia mashabiki wa soka duniani kote.

Ukurasa huu una vipengele vikuu vitano, ambavyo ni Chelsea Habari, Chelsea Usajili, Chelsea HD, Mitandaoni pamoja na Majirani.
  1. Chelsea Habari; hiki ni kipengele maalumu kwa ajili ya kukuletea habari zote zinazoihusu klabu ya Chelsea pamoja na vilabu vilivyochini ya klabu hiyo ambavyo ni klabu za Vijana wa akademi (Chelsea Youth) pamoja na klabu maalumu kwa soka la akina dada (Chelsea Ladies) lakini pia habari za klabu yenyewe ya wanaume (Chelsea FC)
  2. Chelsea Usajili; hiki ni kipengele kinachokuletea habari zote kuhusu tetesi za usajili na hata sajili zilizokamilika kwa wachezaji walionunuliwa ama kuuzwa na Chelsea au hata wanaotajwa kutoka ama kuingia ndani ya klabu hizo.
  3. Chelsea HD; hiki ni kipengele maalumu kwa ajili ya kukuletea matukio yote yaliyotokea klabuni Chelsea
  4. Mitandaoni; kipengele hiki ni maalumu kwa ajili ya kukuletea matukio yote yanayoihusu klabu ya Chelsea na watu wake klabuni hapo katika mitandao ya kijamii.
  5.  Majirani; kipengele hiki ni maalumu kwa kukuletea habari za wachezaji waliopo kwa mkopo kwenye vilabu vyengine wakitokea Chelsea, lakini pia wakongwe na wachezaji wote waliowai kuichezea au kuitumikia klabu ya Chelsea.
Hii ndio nia na mambo yote yanayohusika katika ukurasa huu wa Darajani 1905. Kama unahitaji kutoa ushauri, au kutangaza ama kufanya ya matangazo kupitia ukurasa huu basi wasiliana nasi kwa kubonyeza hapa