Chelsea Women inashuka uwanjani hii leo mara baada ya mchezo uliopita kupata ushindi mnono wa mabao 8-0 dhidi ya wanawake wa West Ham, mchezo uliochezwa jumapili ya tarehe 2-Februari.
Lakini pia kabla ya mchezo huo Chelsea ilimenyana dhidi ya wanawake hawahawa wa Man utd kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Ligi maarufu kama Continental Cup na Chelsea ikatinga hatua ya fainali kwa ushindi wa bao 1-0, bao lililofungwa na nyota mkongwe, Maren Mjelde.
Mchezo wa leo ni mchezo muhimu kwa Chelsea katika mbio zake za kuwania ubingwa wa ligi kuu ambapo kwasasa inashika nafasi ya pili uku ikiwa imecheza michezo pungufu ikizidiwa mchezo mmoja na ratiba inavyotakiwa kuwa ikiwa ina alama 35 uku Man city Women walio kileleni wakiongoza wakiwa wana alama 36.
No comments:
Post a Comment