Chelsea yaingia sokoni kusaka mrithi wa Marcos Alonso na Emerson Palmieri - Darajani 1905

Chelsea yaingia sokoni kusaka mrithi wa Marcos Alonso na Emerson Palmieri

Share This
Chelsea inatajwa kuingia kwenye mpango wa kumsajili nyota beki wa kushoto wa klabu ya Wigan na timu ya taifa ya Marekani, Antonee Robinson.

Nyota huyo mwenye miaka 22 anatajwa kutakiwa na klabu kadhaa ikiwemo Chelsea inayotajwa kwamba ipo tayari kumtoa beki mmojawapo kati ya Marcos Alonso au Emerson Palmieri ili kumsajili kwa mabadilishano na mshambuliaji wa Inter Milan, Lautaro Martinez

Kwenye usajili huu wa Antonee, Chelsea inaweza kumtumia mmarekani mwenzake, Christian Pulisic kama ushawishi kwa beki huyo.

No comments:

Post a Comment