Mara baada ya mchezo wa ngwe ya kwanza ya klabu bingwa barani Ulaya kati ya Chelsea dhidi ya Barcelona ambao mchezo huo uliisha kwa sare ya mabao 1-1 ambapo Willian ndiye aliyechaguliwa kuwa nyota wa mchezo huku akiifungia goli moja klabu hiyo, nyota mwenzake klabuni hapo, Eden Hazard alieleza ni nini alichomwambia mchezaji huyo mara baada ya kipindi cha kwanza kuisha.
"Nilimwambia hatakiwi kugongesha mwamba, na badala yake apige ili afunge na kweli alifanya hivyo. Nilimwambia hivyo katika kipindi cha kwanza, na kipindi cha pili alifanya kama nilivyomwambia na akafunga. Ye ni mchezaji bora mwenye uwezo mkubwa, na ilo ametuonyesha, " alisema nyota huyo.
"Inatakiwa tuwe na ubora zaidi, tunatakiwa kucheza tuiwa na uhakika wa
kutokuruhusu kufungwa na inatakiwa tufunge ili tuweze kusonga mbele.
Bado tuna wiki tatu za kujiandaa kabla ya kucheza marudiano (dhidi ya
Barcelona) na tutapambana kupigania nafasi yetu" alisema nyota huyo
alipoulizwa juu ya nafasi ya Chelsea kufudhu kucheza hatua ya robo
fainali ambapo mchezo wa marudiano utachezwa siku ya tareh 14-Marchi
huko nchini Hispania.
HAZARD AELEZA ALICHOMWAMBIA WILLIAN
Share This
Tags
# Chelsea FC
# Chelsea Habari
Share This
About Darajani 1905
Chelsea Habari
Labels:
Chelsea FC,
Chelsea Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment