Klabu ya Chelsea inatajwa kumfukuzia nyota kuutoka klabu ya As Roma ya nchini Italia, Frorenzi. Ambaye amebakisha mkataba wa mwaka mmoja ili kumalizana na klabu yake hiyo. Frorenzi ambaye ni raia wa Italia anatajwa kutakiwa na Chelsea kwa karibu huku akitajwa kuondoka klabuni hapo katika dirisha kubwa la usajili.
Klabu kadhaa zinatajwa kuonyesha nia ya kumtaka kiungo huyo mwenye uwezo pia wa kucheza kama mlinzi wa kati, ila Chelsea sasa ndio imeanza kutajwa kwa karibu kumnasa ikipambana na klabu za Juventus pamoja na AC Milan ambazo nazo zinamtaka nyota huyo mwenye miaka 26.
Kama Chelsea ikifanikiwa kumnasa nyota huyu, itakuwa imetimiza wachezaji watatu kuwanasa kutokea kwenye klabu hiyo toka Chelsea ilipokuwa chini ya kocha muitaliano, Antonio Conte. Wachezaji waliotoka kwenye klabu hiyo ambao tayari wameshatua Chelsea toka kuwepo kwa Conte ni pamoja na Antonio Rudiger pamoja na Emerson Palmieri.
CHELSEA KUMNASA MWENGINE KUTOKA AS ROMA
Share This
Tags
# Chelsea Usajili
Share This
About Darajani 1905
Chelsea Usajili
Labels:
Chelsea Usajili
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment