Eden Hazard, nyota wa Chelsea mwenye miaka 27 ambaye ni raia wa Ubelgiji naye amefanikiwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tunzo ya mchezaji bora kwa mwezi Februari akiiongoza vyema klabu yake katika michezo ya ligi kuu kwa mwezi huo.
Katika mwezi huo, aeiongoza Chelsea katika michezo mitatu ya ligi kuu huku akifanikiwa kuiongoza kushinda mchezo mmoja dhidi ya West Bromwich ambapo mwenyewe alifunga magoli mawili na kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo. Lakini pia katika mwezi huo akifunga magoli matatu na kuteneza nafasi 11.
Wengine anaoshindana nao katika kipengele hicho;
- Sergio Aguero-Man city
- Moussa Dembele-Tottenham
- Pascal gross-Brighton
- Glenn Murray-Brighton
- Mohammed Salah-Liverpool
- Xherdan Shaqiri-Stoke city
No comments:
Post a Comment