RASMI; CHELSEA YAPANGIWA MCHEZO WA NUSU FAINALI - Darajani 1905

RASMI; CHELSEA YAPANGIWA MCHEZO WA NUSU FAINALI

Share This
Kikosi cha vijana cha Chelsea kilichochini ya kocha Jody Morris kitasafiri kuifata klabu ya vijana ya Birmingham City siku ya tarehe 04-Aprili ili kucheza mchezo wa nusu fainali ya kombe la FA, ambapo mchezo huo umepangwa kuchezea mishale ya saa 22:00 kwa saa za Afrika Mashariki. Tiketi kwa ajili ya mchezo huo zitauzwa siku hiyo getini ambapo kiingilio kwa watu wote ni paundi moja (Tsh.3,000) ambapo huo utakuwa ni mchezo wa kwanza huku mchezo wa pili yaani mchezo wa marudiano ukitarajiwa kuchezwa Stamford Bridge.

Kama Chelsea ikifanikiwa kushinda michezo nusu fainali pamoja na fainali ya michuano hiyo basi itafanikiwa pia kuweka rekodi ya kutwaa taji hilo mara tano mfululizo ambapo mpaka sasa imeshashinda michuano hiyo mara nne huku ikifanikiwa kuweka rekodia kufika hatua ya nusu fainali mara tisa mfululizo katika kombe hilo la FA.

Lakini pia hii ni mara ya pili mfululizo, Chelsea inamenyana dhidi ya Birmingham ambapo mwaka jana mwezi Januari, Chelsea iliibamiza klabu hiyo katika hatua ya raundi ya nne kwa magoli 5-0 ambapo magoli ya Chelsea yalifungwa na Mason Mountambaye alifunga magoli matatu na kwa sasa anaichezea klabu ya Vittese kwa mkopo, Reece James pamoja na Cole da Silva.

No comments:

Post a Comment