Chelsea inataka kumsajili tena nyota huyo kinda ambapo dau la paundi milioni 12 linatajwa kutumia kumsajili nyota huyo aliyekuwa mchezaji wa Chelsea kabla ya kujiunga na Sassuolo mwaka 2018 akiondoka Chelsea aliyoichezea mchezo mmoja.
Taarifa zinazoripotiwa na magazeti kadhaa ya barani Ulaya ni kwamba mkurugenzi wa michezo na mwenyekiti wa bodi ya Chelsea, Marina Granovskaia leo atakutana na uongozi wa klabu ya Sassuolo ili kukamilisha biashara ya nyota kinda wa klabu hiyo, Jeremie Boga.
No comments:
Post a Comment