Lampard na Marina watunishiana misuli kisa ubora wa Arrizabalaga - Darajani 1905

Lampard na Marina watunishiana misuli kisa ubora wa Arrizabalaga

Share This
Kwa taarifa za chini chini, zinazoripotiwa na vyanzo kadhaa zinadai klabuni Chelsea kuna mzozo mkubwa unaoendelea kati ya kocha Frank Lampard na mkuu wa bodi ya Chelsea, Marina Granovskaia anayetimiza pia majukumu ya mkurugenzi wa michezo.


Taarifa hizo zinadai kwamba Frank Lamard haridhishwi na ubora wa kipa huyo raia wa Hispania mwenye miaka 25 na anataka nyota huyo auzwe kwenye dirisha kubwa lijalo wakati Marina Granovskaia ambaye alikamilisha uhamisho wa kipa huyo kutoka Athletico Club akitaka kipa huyo aendelee kupewa nafasi.


Mjadala huu unatajwa kuleta mitazamo tofauti kati ya kocha ambaye inaonekana imani yake kwa kipa huyo imeshuka kabisa pamoja na mkurugenzi wa michezo anayehusika na usajili klabuni hapo.

No comments:

Post a Comment