Taarifa hiyo imetolewa na rais mpya wa chama cha soka cha nchini Italia (FIGC), anayeitwa Roberto Fabricini akisema kocha Antonio Conte anatamani kurudi kwenye timu ya taifa ya nchi hiyo "Majina yanayoweza kuchukua majukumu hayo huenda akawa Roberto Mancini ambaye alikuwa Roma ingawa hatujafanya mawasiliano naye, Conte ni kama anatamani kurudi tena kuifundisha timu ya taifa, Carlo Ancellotti ni kama alifungua milango ila baadae akaifunga na hata Claudio Ranieri inaonekana hapatikani" alisema rais huyo alipoulizwa ni nani atachukua nafasi ya ukocha katika timu ya taifa ya nchini humo. Ambapo timu hiyo kwa sasa haina kocha kutokana na kocha aliyekuwepo Gian Piero Ventura kuachana na timu hiyo mara baada ya kushindwa kuisaidia kufuzu kucheza kombe la dunia mwaka huu uko nchini Urusi.
Kocha Antonio Conte aliwai kuifundisha Italia toka mwaka 2014 mpaka mwaka 2016 ambapo kuanzia hapo akatangazwa rasmi kuwa kocha wa Chelsea.
No comments:
Post a Comment