Usiku wa leo majira ya saa nne Chelsea Women itarejea uwanjani mara baada ya mchezo uliopita kuhairishwa kutokana na hali mbaya ya hewa.
Leo Chelsea Women itakuwa nyumbani Kingsmeadow kucheza mchezo wake wa ligi kuu Uingereza kwa soka la wanawake maarufu kama Barclays FA WSL ambapo wataikaribisha klabu ya wanawake ya Birmingham.
Mchezo huo ni nafasi kwa Chelsea kuzidi kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa ligi hiyo ambapo wanakimbizana kwa karibu na Man city Women na Arsenal Women.
No comments:
Post a Comment