Lakini wakati Chelsea ikiwa inashuka uwanjani usiku wa leo, basi pia itakuwa inakumbuka siku ya kuzaliwa ya gwiji wa soka klabuni hapo, Peter Osgood ambaye alizaliwa siku kama ya leo miaka 71 iliyopita ingawa aliaga dunia akiwa na miaka 59, yaani alifariki miaka 12 nyuma (Mwaka 2006).
Gwiji huyo wa soka alikuwa na historia kubwa klabuni Chelsea mpaka kutajwa moja ya wakongwe na magwiji wasiokuja kusahaulika klabuni Chelsea huku katika uwanja wa Stamford Bridge ikiwekwa sanamu yake. Alicheza Chelsea kwa vipindi viwili tofauti huku akicheza michezo 289 na kufunga magoli 105.
Roho yako ilazwe mahali pema peponi, Amen!
No comments:
Post a Comment