"Kama ukiniuliza ni wachezaji gani raia wa Uingereza ambao nilivutiwa nao sana pindi nilipocheza nao nitakutajia John Terry, Steven Gerrard, Wayne Rooney na Frank Lampard."
.
"Lakini ukiniuliza nyota ambao sio waingereza ambao nilivutiwa nao pindi nilipocheza nao nitakutaji Arjen Robben na Eden Hazard. Na hapo ndipo napojivunia kwa kucheza na nyota bora wenye akili ya mpira."
.
"Lakini kama ukiniambia nimchague mchezaji mmoja ambaye kwangu namuona ni bora zaidi ambaye niliwai kucheza nae ni Eden Hazard."
.
"Anakila kitu ambacho mchezaji bora anatakiwa awe nayo. Nilicheza nae Lille akiwa ana miaka 19 lakini ilikuwa ukimtazama unasema kweli huyu ni mchezaji kamili." amesema winga na nyota wa zamani wa Chelsea, Joe Cole.
.
Inamaana Cole anamaanisha akina Drogba na Lampard hawajafikia uwezo wa Hazard? je ni kweli? embu weka mtazamano wako hapo.
Umemsikia alichokisema Joe Cole kuhusu Eden Hazard?
Share This
Tags
# Chelsea FC
# Chelsea Habari
Share This
About Darajani 1905
Chelsea Habari
Labels:
Chelsea FC,
Chelsea Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment