Lampard kuingia sokoni kumsaka kipa wa kumrithi Kepa - Darajani 1905

Lampard kuingia sokoni kumsaka kipa wa kumrithi Kepa

Share This

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Star limeripoti kwamba kocha Frank Lampard haridhishwi na kiwango na uwezo wa kipa nambari moja klabuni hapo, Kepa Arrizabalaga.

Hivyo kuna taarifa kwamba kocha huyo ameingia sokoni kumnasa kipa atakayeziba pengo la mlinda mlango huyo mwenye miaka 25 kutoka nchini Hispania.


Kipa Nick Pope wa Burnley ambaye ni raia wa Uingereza anatajwa kuwepo kwenye kinyang'anyiro hicho cha kuwaniwa na klabu hiyo ambayo inategemewa kuwa na mabadiliko makubwa kwenye dirisha kubwa la usajili lijalo.

Lakini pia kipa wa Crystal Palace, Vicente Guaita ambaye ni raia wa Hispania anatajwa pia kutakiwa na klabu hiyo inayopatikana kusini-magharibi mwa jiji la London.


No comments:

Post a Comment