Mikel akutana na dhahma Uturuki - Darajani 1905

Mikel akutana na dhahma Uturuki

Share This
Nyota wa  zamani wa Chelsea, John Obi Mikel amekutana na dhahma huko nchini Uturuki akiwa anaitumikia klabu yake ya Trabzonspor kwenye mchezo wa ligi kuu nchini humo dhidi ya Fenerbahce jumamosi iliyopita.


Mchezo huo ulioisha kwa Trabzonspor kushinda 2-1 ukiwa ni mchezo wenye upinzani mkubwa ndani ya uwanja na nje ya uwanja, nyota huyo raia wa Nigeria alipata dhahma ya kubaguliwa rangi na mashabiki wa timu pinzani na klabu yake ya Trabzonspor imethibisha kwamba kesi hiyo imepelekwa kwenye vyombo vya sheria kuwashtaki mashabiki wa timu pinzani.


Inaelezwa kwamba Obi Mikel amekuwa akipokea jumbe za ubaguzi wa rangi na kusemwa vibaya lakini pia kundi la mashabiki wachache wakimfata na kumbagua waziwazi.


Nyota huyo mwenye  miaka 32 anadai pia ubaguzi huo umewakumba pia familia yake ambayo inamjumuisha mke mmoja na watoto wawili wakike.


No comments:

Post a Comment